Jinsi tukio lilivyokuwa
Nasri, ambaye anacheza kwa mkopo kwenye timu ya Sevilla ya Hispania kutoka Manchester City ya Uingereza, alipewa kadi nyekundu katika dakika ya 74, kwa kumpiga kichwa Vardy baada ya wachezaji hao, kugombana walipokuwa bila ya mpira.
Leicester iliwatoa mabingwa hao, wa Europa League wa msimu uliopita, kwa jumla ya mabao 3-2, kwenye mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa King Power, na mbweha hao kutinga robo fainali ya ligi ya mabingwa Barani Ulaya kwa mara ya kwanza.
"Kwa mimi yeye ni mwongo kwa sababu kama angekuwa mchezaji wa kigeni, nyinyi waandishi wa Uingereza, mngesema kuwa ni mwongo, kwa mimi yeye (Vardy) ni mwongo," alisema kiungo huyo wa zamani wa Arsenal.

