Simba Queens
Kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Sebastian Nkoma kimeanza maandalizi mapema ili kuhakikishia tunakwenda kufanya vizuri kwenye michuano hiyo mikubwa barani Afrika.
Katika maandalizi hayo, leo saa 10 jioni kikosi kitafanya mazoezi katika Uwanja wa Mo Arena na baada ya hapo kitaingia kambini moja kwa moja.
Queens ambayo inawakilisha Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) imepangwa Kundi A pamoja na timu za Afsa FC (Morocco), Green Buffalo (Zambia) na Determine Girls (Libya).