Jumatatu , 25th Sep , 2023

Mkufunzi wa Chelsea Mauricio Pochettino amesema timu yake inapaswa kukua na kucheza kama timu moja baada ya kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Aston Villa kwenye mchezo wa ligi kuu ya England EPL uliochezwa Jumapili ya Septemba 24-2023.

Pochettino amesema tunapaswa kukua kama timu pamoja na sio kwa mtu binafsi  maana kwa aina hii ya uchezaji tunapaswa kushindana na kushinda michezo kwa kuwa mchezo wa soka ni kushinda ndio maana tunahuzunishwa na hali mbaya tunayopitia kwa sasa.

Chelsea inashika nafasi ya 14 kwenye msimamo wa EPL wakishinda mchezo 1 pekee kwenye michezo 6 na kuwa msimu mbaya zaidi kwao tangu mwaka 1978 huku jumatano Septemba 27-2023 watacheza na Brighton& Hove Albion kwenye kombe la Carabao Cup