Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Spika Ngudai amtupia kijembe Mwigulu kuhusu Yanga

Jumatatu , 12th Apr , 2021

Kufuatia klabu ya Yanga kutoka sare ya goli 1-1 dhidi ya KMC kwenye mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara siku ya Jumamosi kwenye uwanja wa Mkapa, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai amemtupia kijembe Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Mwigulu Nchemba.

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Mwigulu Nchemba (kushoto) na Spika wa Bunge Job Ndugai

Spika Ndugai ameanzisha utani huo leo Aprili 12, 2021, bungeni kwenye kikao cha 7, mkutano wa 3 wa bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo amesema wachezaji wa Yanga SC wana njaa hivyo angalau wabunge wawachangie.

"Jana nilimtafuta Waziri wa Fedha Mhe. Mwigulu Nchemba kwa mambo yetu haya ya bunge akaniambia Spika tafadhali niache, nikauliza sasa nakuacha kuna nini tena? akasema nina 'stress', kumbe matokeo ya juzi yamempa 'stress', pole Mhe. Nchemba na wanayanga wote," - Spika Ndugai

Spika Ndugai akaongeza kwa kusema kuwa, "Taarifa tulizonazo wachezaji wana njaa, maana wamelegea legea hivi, kwa hiyo waheshimiwa wabunge baadaye tunaweza kufanya mchango kidogo tuwasaidie Yanga."

Baada ya sare hiyo, Yanga SC imefikisha pointi 51 baada ya kucheza michezo 24 huku Azam FC wakiwa nafasi pili na pointi 47 ikiwa imecheza michezo 25 na mabingwa watetezi Simba SC wakiwa na pointi 46 wakiwa wamecheza michezo 20.
 

Tazama Video hapo chini
 

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi