Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwamuzi wa mpira auawa kwa risasi

Ijumaa , 18th Aug , 2017

Mwamuzi maarufu katika mchezo wa kandanda nchini Somalia amepigwa risasi na kuuawa karibu na nyumbani kwake mjini Mogadishu wakati akirejea nyumbani kwake mtaa wa Wardhigley akitokea msikitini.

Taarifa zinasema kuwa mwamuzi huyo Osman Jama Dirah, ambaye alisimamia mechi za kanda na kimataifa ameuawa na wanaume wawili waliomfyatulia risasi kadhaa pasipo kugundulika chanzo cha watu hao kufanya hivyo. 

Mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Somalia Anas Ali Mohamud amenukuliwa akisema aliwaona washambuliaji wakiondoka eneo la mauaji na baadaye maafisa wa usalama walifika eneo hilo  lakini kufikia hawajafanikiwa kuwakamata wahusika.

Kwa mujibu wa mwandishi wa BBC Somali Ahmed Adan anasema kuuawa kwa Osman Jama Dirah ni pigo kubwa kwa tasnia ya soka nchini Somalia pamoja na sekta yote ya michezo nchini humo.

Osman Dirah alikuwa miongoni mwa marefa maarufu zaidi nchini humo tangu kusambaratika kwa serikali kuu miaka 27 iliyopita na alifahamika kama mwamuzi bora zaidi na alihudumu katika kamati ya waamuzi katika Shirikisho la Soka la Somalia.

Dirah alianza kushiriki katika kandanda mwaka 1979, kama mlinda lango wa timu ya Galgadud, na baadaye akajiunga na timu ya taifa kama mlinda lango huku mwaka 1997 akiteuliwa kuwa mwamuzi na FIFA nchini Somalia.

 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi