
Hatua ya penati ilifikiwa baada ya timu zote mbili kutoa sare ya bao 1-1 katika dakika 90 ya mchezo ambapo Tanzania ndio walioanza kujipatia bao lake la kwanza kupitia kwa John Bocco katika dakika ya 25 ya mchezo.
Kipindi cha kwanza cha mchezo kilikamilika huku Tanzania ikiwa mbele kwa bao 1-0 dhidi ya Ethiopia lakini katika kipindi cha pili cha mchezo Ethiopia ilijipatia bao lake la kusawazisha ndani ya dakika ya 57 kupitia kwa Gatoch Panom hivyo kupelekea timu zote kuwa sare ya bao 1-1 mpaka dakika 90 za mchezo.
Akizungumza baada ya mechi hiyo, kocha mkuu wa The Kilimanjaro Stars Abdallah Kibaden amewalalamikia waamuzi katika mchezo huo kuwa wamechangia wao kushindwa kusonga mbele katika michuano hiyo.