Jumatano , 2nd Apr , 2014

Bondia namba moja Tanzania kwa uzito wa Bantam, Francis "Chichi Mawe" Miyeyusho, amesema huwa hana muda wa kupoteza kutaka kujua mbinu za mpinzani wake na badala yake yeye hujifua kwa bidii ili kuweza kumdhibiti kwa namna yoyote.

Francis 'Chichi Mawe' Miyeyusho(aliyevua shati)

Francis Miyeyusho atapanda ulingoni Jumamosi hii kwenye ukumbi wa Karume ndani ya viwanja vya maonesho ya biashara vya mwalimu Nyerere kupambana na Ronald Pontillas wa Ufilipino.

Awali Francis Miyeyusho alinukuliwa akikataa kupigana katika pambano hilo kabla ya kubadilisha uamuzi wake na kutangaza kwamba atapanda ulingoni siku hiyo.