Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Makapteni watunishiana misuli

Jumatano , 30th Aug , 2017

Ikiwa zimebakia siku mbili vumbi kutimka katika michuano ya Sprite BBall Kings hatua ya mwisho ya fainali, manahodha wa timu shiriki wameanza kutunishiana misuli kwa kila mmoja kujivutia kwake kuwa atakinyakuwa kikombe cha mashindano hayo.

Akizungumza nahodha wa timu ya TMT, Isihaka Masoud amesema wamejifua vizuri katika kuelekea mechi hiyo huku akidai 'game' hiyo itakuwa yenye ushindani mkubwa kwa kuwa kila mmoja amejipanga kupata matokeo yaliyokuwa mazuri.

"Nina imani mechi ijayo (game 5) ya fainali za Sprite BBall Kings itakuwa nzuri kwa sababu timu yetu imejiandaa vizuri. Safari hii tutakuja tofauti kwa kuwa tunapitia 'step' zote tulizozipitia katika michuano hii",alisema Masoud.

Kwa upande wake nahodha wa Mchenga BBall Stars, Mohamed Yusuph 'Muddy' amesema timu yake imejiandaa vizuri katika kupambana na wapinzani wao huku akijitapa kwa kuwataka mashabiki zao wajitokeze kwa wingi kushuhudia wanavyo kibeba kikombe chao.

"TMT wamechelewesha ubingwa tu ila sisi nafasi yetu iko pale pale katika kukinyakua kikombe. Tunawalika mashabiki wetu wote waje kwa wingi kushuhudia 'basketball inavyochezwa na Mchenga kwa kuwa tumejipanga kuchukua ubingwa asubuhi kweupee", alisema Muddy.

Mchenga BBall Stars na TMT wanakutana tena kwa mara ya mwisho Septemba 2 mwaka huu katika mechi ya mwisho ya fainali za Sprite BBall Kings 'game 5' zitazopigwa katika viwanja vya Don Bosco Oysterbay Jijini Dar es Salaam ambapo mechi hiyo ndiyo itakayoweza kumtambulisha mshindi rasmi wa michuano ya Sprite BBall Kings kwa mwaka 2017.

HABARI ZAIDI

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross