Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Huu msiba ni mzito" - Mo Dewji, Mzee Yusuph,GNako

Ijumaa , 24th Jul , 2020

Siku ya Julai 24, 2020 inaingia kwenye kumbukumbu ya Taifa kwa kumpoteza Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa, aliyeiongoza Tanzania kuanzia mwaka 1995 hadi 2005 na alizaliwa Novemba 12,1938.

Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin William Mkapa aliyefariki dunia usiku wa kuamkia Julai 24, 2020

Baadhi ya watu maarufu hapa nchini kuanzia wanasiaisa, wafanyabiashara, na wasanii wameonesha hisia zao kwa kuguswa na msiba huu na kueleza namna gani ambavyo wanamkumbuka Benjamin William Mkapa kupitia mitandao ya kijamii.

"Bado ni ngumu kukubali kwamba Mzee Mkapa hatunaye tena, pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania kwa ujumla kwa msiba huu mzito, Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahali pema peponi, tangulia Baba, nasi tunakuja" ameandika Mfanyabiashara na Mwekezaji wa Klabu ya Simba Mo Dewji.

"Kwake tumetoka na kwake tutarejea, watanzania sote tutakukumbuka upumzike kwa amani Mstaafu Rais wetu" ameandika Msanii Mzee Yusuph

"Tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba wa kiongozi wetu, mlezi wetu na Rais wetu mstaafu Mh Benjamin William Mkapa, salam za pole ziwafikie ndugu jamaa na marafiki wa marehemu popote pale walipo, tupo pamoja nanyi katika kipindi hiki kigumu na Mungu awatie nguvu" ameandika G Nako Warawara.

"Habari ya kusikitisha sana ambayo nimeamka nayo, Tumempoteza Rais wa awamu ya tatu Tanzania Benjamin William Mkapa, pumzika kwa nguvu ahsante kwa diplomasia yako, mchango wako na huduma zako kwenye jamii" ameandika  Nikki Mbishi.

"Nilipokea habari za Rais Benjamin Mkapa kwa huzuni kubwa, mtu wa kanuni, dhamira thabiti na uadilifu, rehema yangu kwa familia yake, marafiki, wanachama wa Chama cha CCM, na Tanzania nzima kwa ujumla, pumzika kwa amani Mzee Mkapa" ameandika Wakazi.

 

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi