Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Hata Mungu anaipenda siasa - Dkt. Mashinji

Jumamosi , 5th Nov , 2016

Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Vincent Mashinji, ameonesha kupingana na baadhi ya watu wanaodai kuwa siasa ni mchezo mchafu, kwa kusema kuwa dhana hiyo siyo sahihi kwa kuwa hata Mwenyezi Mungu aliyeumba kila kitu, anaipenda na ndiyo maana akairuhusu.

Dkt. Vincent Mashinji - Katibu Mkuu CHADEMA

 

Dkt. Mashinji alitoa kauli hiyo hivi karibuni kupitia kipindi cha KIKAANGONI kinachurushwa kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV, ambapo mwananchi mmoja alitaka kujua mtazamo wake kuhusu dhana ya siasa kuwa mchezo mchafu na ni kwanini yeye aliamua kuingia kwenye siasa wakati akijua kuwa ni mchezo mchafu.

"Siasa siyo mchezo mchafu, hata kwa Mungu kuna siasa na ndiyo maana kulikuwa na utawala, hata yeye anapenda siasa ndiyo maana ameileta, siasa ni mfumo wa maisha, na ndiyo maana hakuna jambo lolote la maendeleo litaweza kufanyika bila siasa, siasa ni mfumo wa uongozi, siyo kweli kuwa siasa ni mchezo mchafu" Alijibu Dkt. Mashinji.

Aidha Mashinji ambaye ni daktari wa binadamu, amesema aliingia kwenye siasa miaka mingi iliyopita, na kwamba siyo mgeni kama ambavyo watu wengi wanadhania na kuongeza kuwa awali alikuwa ni mwanachama wa CCM lakini alipoona anaweza kuwa kiongozi na kusaidia maendeleo alijiunga na CHADEMA kwa kuamini kuwa ni chama kinachoweza kuliletea taifa maendeleo.

"Nimewahi kuwa mwanachama wa CCM, lakini ni katika kipindi ambacho ilikuwa ni lazima uwe na kadi ya CCM ili upate huduma au fursa fulani, kwahiyo nilikuwa na kadi lakini sikuwa na mapenzi na CCM" Alisema Dkt Mashinji na kuweka wazi kuwa yeye bado ni mwanataaluma katika fani ya udaktari na pia ni mtendaji wa chama ambaye hahitaji kuwa mtu wa majukwaani bali mtu anayefanya kazi kimyakimya.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi