Jumanne , 8th Apr , 2014

Baada ya msanii wa Kenya, Wyre The Love Child kufanikisha kolabo za kimataifa zenye mafanikio makubwa katika muziki wake, zikiwepo kazi alizofanya na Alaine pamoja na Cecile, msanii huyu ametajwa kuwa katika mchongo wa kufanya kazi na msanii Konshens

Wyre

Wyre anatarajiwa kuchukua hatua hii hivi karibuni wakati Konshens atakapotua nchini Uganda kwa ajili ya onesho mwishoni mwa wiki, taarifa zinazopewa nguvu na Kauli ya kipindi cha nyuma ya staa huyu kutoka Jamaica kuwa anakubali sana kazi za Wyre.

Endapo mipango hii itakwenda sawa sawa, hii itakua ni hatua nzuri ya kuanza mwaka kwa kolabo nyingine ya kimataifa kwa msanii Wyre ambaye soko la muziki wake nje ya Kenya limekuwa likendelea kukua siku hadi siku.