Jumatatu , 17th Mar , 2014

Msanii Sir Tino kutoka Seductive Records akishirikiana na Ssen Lubi watoa ngoma ya “Penzi La Star”, ambayo inatangulia filamu ambayo itasimama kwa jina 'Penzi la Star'.

Video hii ambayo imefanyika chini ya Muongoza video Mahiri, Solomon Lamba kutoka Emptysouls, mbali na upangiliwaji mzuri wa matukio ndani yake, pia inamhusisha vizuri msanii mwenye 'vocal' matata kabisa Tanzania, Vumilia, na kupitia eNewz ndiyo unaiona kwa mara ya kwanza kabisa leo.

eNewz tumekutana na Tino na hapa anatueleza mwenyewe kuhusu video hii.