![](http://eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2018/12/19/MWANA FA.jpg?itok=GGwM-EB-×tamp=1545236037)
Kushoto ni Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na kulia ni msanii Mwana FA.
Kikwete ameeleza hayo leo baada ya kutembelewa na Mwana FA nyumbani kwake kwa lengo la kumuonesha bidhaa yake hiyo mpya inayoitwa 'Fyn By Falsafa'.
''Kuna siku nilimsihi Mwana FA na wanamuziki wengine kufanya shughuli nyingine zaidi ya muziki pekee'', ameandika Kikwete kwenye ukurasa wake wa Twitter.
Mstaafu huyo alieyongoza kutoka mwaka 2005 hadi 2015, ameongeza. ''Nimefarijika leo kunitembelea na kutambulisha bidhaa yake mpya ya “body spray”. Hii ni hatua kubwa na nzuri kwa vijana wetu. Tuwaungishe!''.
Kuna siku nilimsihi @MwanaFA na wanamuziki wengine kufanya shughuli nyingine zaidi ya muziki pekee. Nimefarijika leo kunitembelea na kutambulisha bidhaa yake mpya ya “body spray”. Hii ni hatua kubwa na nzuri kwa vijana wetu. Tuwaungishe! pic.twitter.com/zqpE4e6UGk
— Jakaya Kikwete (@jmkikwete) December 19, 2018
Mwana FA ni miongoni mwa wasanii mbalimbali ambao wametengeza bidhaa nje ya muziki na sanaa nyingine akiwemo Flaviana Matata ambaye anauza rangi ya kucha iitwayo Lavy pamoja na Jux ambaye anauza nguo kupitia 'brand' yake ya African Boy.