Jumamosi , 2nd Jan , 2016

Mwanamuziki alieanzia katika miziki ya Kizazi Kipya baadae muziki wa band ,Mwanadada Leah Muddy kwa sasa ameugeukia muziki wa Injili na amesema amekwisha achia album yake ya Namshangaa bwana Mungu maalumu kama zawadi yake ya mwaka 2016.

Mwanamuziki wa Injili Leah Muddy

Mwanamuziki huyo ambae awali alitokea katika mashindano ya kuibua vijana nchini amesema ameamua kuimba injili ili kuwa karibu na mungu kwa kuwa kwa sasa ameamua kubadilisha style ya Maisha yake.

Leah Muddy amesema ametumia mitindo tofauti katika album yake hiyo ambapo amesema kwa sasa yupo katika mchakato wa kukamilisha video za nyimbo zote zilizopo kwenye album hiyo kwa ajili ya kuipa nguvu zaidi na kueleweka kwa mashabiki.