Jumatatu , 15th Jun , 2015

Star wa vichekesho wa nchini Uganda, Anne Kansiime amechaguliwa kuendesha sherehe za ugawaji tuzo za kubwa za AFRIMMA kwa mwaka huu, tukio ambalo litafanyika Oktoba 10 huko Dallas Texas nchini Marekani.

Kansiime atafanya shughuli hii sambamba na mchekeshaji mwingine mkubwa Afrika, bascketmouth kutoka nchini Nigeria ili kuongeza ladha zaidi katika sherehe hizo kwa mwaka huu.

Hii inakuwa ni nafasi nyingine kubwa kwa mchekeshaji huyo kuendelea kutangaza sanaa yake na vile vile kupeperusha bendera ya nchi yake kimataifa, kufuatia taarifa hii ambayo pia imethibitishwa na Johnson Mujungu ambaye ni meneja wake.