Picha ya pamoja Bebe Cool na Zuena Kirema
Ni muda sasa umepita tangu Bebe amemuahidi mkewe Zuena kufunga nae harusi kubwa na ya kifahari na huwenda ndoto hiyo ya muda mrefu ikatimia baada ya kuonesha shauku kubwa ya kumpa Zuena harusi ya ndoto yake.
Msanii huyo wa Uganda ametumia mtandao wake wa instagram kuelezea hisia zake kwa kusema "Jumamosi, nilitumbuiza kwenye harusi ya rafiki yangu King Ivan Goodheart na ilinifanya nisisimke zaidi kuhusu siku ya harusi, Mwenyezi Mungu anilinde mimi, mke wangu, familia, na marafiki ili tuweze kuishi na kuona siku hiyo’’.