Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wananchi waua wakiisaidia polisi

Jumatano , 11th Oct , 2017

Jambazi mmoja ameuawa na wananchi wakati akiwatoroka askari baada ya kubainika kufanya jaribio la kutenda uhalifu katika mradi wa ujenzi wa kituo cha pamoja cha forodha OSBP Tunduma mkoani Songwe.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi kamishna msaidizi wa polisi mkoa wa Songwe amesema tarehe 10 usiku wa kuamkia jumatano hii majambazi hao walipanga kufanya tukio la uhalifu katika mradi wa ujenzi wa kituo cha forodha OSBP

Tunduma na kwamba baada ya kugundulika walikimbia na kutelekeza bunduki yenye risasi 30, na zana zingine walizokuwa nazo.

Kamanda Nyange amesema majambazi wawili walifanikiwa kutoroka wakati mmoja aliyetajwa kwa jina la Isha Martin Mwampulo (20) mkazi wa Lwasho kata ya Ndalambo wilayani Momba akinaswa na wananchi, ambapo hata hivyo baada ya kushambuliwa alijeruhiwa vibaya na kufariki dunia akiwa njiani kuwahishwa hospitali.

Wakazi wa mji wa Tunduma mbali ya kupongeza jitihada za jeshi la polisi, wamesema wako tayari kushiriki kikamilifu katika kufichua wahalifu lakini wakataja kasoro ya askari kuchelewa kufika pindi wanapoarifiwa kuhusu uhalifu jambo linalowakatisha tamaa wananchi katika kushiriki kupambana na uhalifu.

Aidha jeshi la polisi limedai kuwa jambazi huyo alikuwa amevaa sare za wakandarasi na kutumia mwanya huo kutaka kutekeleza azma yake.

Kamanda nyange ameendelea kutahadharisha kuwa Mkoa wa S ongwe sio mahali salama kwa wahalifu na kupongeza ushirikiano wa wananchi kwa jeshi la polisi hadi hivi sasa

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi