Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wananchi wa Lindi waomba kujengewa makazi

Ijumaa , 29th Mar , 2024

Kutokana na Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha na kuharibu nyumba na mashamba ya wananchi wilayani Nachingwea Mkoani Lindi, wananchi wa kata ya Naipanga moja kati ya kata 11 zilizoguswa na kadhia hiyo ya mvua kubwa na madhara yake, wameiomba serikali iwakumbuke.

Nyumba iliyobomolewa na mvua Lindi

Wananchi hao wameomba serikali iwasaidie ili waweze kuishi kwenye makazi salama lakini pia iwasaidie chakula kwani kwa sasa wamekuwa wakilia njaa.

Wakizungumza na EATV wananchi wanasema mvua mfululizo ndio chanzo cha matatizo, kwa sasa hawana makazi na wengi wao wamekuwa wakilala kwenye masalia ya makazi yaliyoharibika ambayo ni hatari huku wengine wakiomba hifadhi kwa ndugu na majirani au hata kulala nje.

“Tumepatwa na maafa makubwa kutokana na mvua kubwa iliyonyesha, kijiji hiki tu kina kaya wastani wa 330, zaidi ya kaya 100 zimeangukiwa na nyumba, katika hao asilimia kama 50 wanaishi kwenye nyumba za kuomba na hizo nyumba zenyewe ni mbovu kwahiyo siku si nyingi aliyeombwa kukaa atatoka na aliyeomba kukaa atatoka” - Thobias Hokororo Mwenyekiti wa kijiji cha Nagaga.

Mvua kubwa hazijaharibu makazi tu kwani hata chakula na vitu vya thamani ambavyo wangeweza kubadilisha kuwa fedha vimekwenda na maji huku mashamba nayo wakilalamika kuwa yamesafishwa hivyo hawajabakiwa na chochote kinachoweza saidia matumbo yao.

Serikali kupitia Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea Mohammed Moyo imeendelea kutoa tahadhari kwa wananchi kutokaa kwenye nyumba zilizobomoka au kuweka nyufa kwani jambo hilo linahatarisha usalama wa maisha yao huku mikakati kama kufanya tathmini ya gharama za maafa, kutoa elimu ya ujenzi bora kwa wakazi wa nachingwea ili kuepusha adha ya nyumba kuharibika nyakati za mvua zikiendelea kutolewa.
 

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi