Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tulia Ackson aeleza kuhusu kugombea Mbeya Mjini

Jumatatu , 19th Aug , 2019

Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Dkt. Tulia Ackson, amesema anampango wa kugombea Ubunge katika uchaguzi mkuu wa 2020, lakini hajabainisha atagombea jimbo gani, kwa kile alichodai chama chake cha CCM, kinamzuia kutaja jimbo atakalogombea.

Naibu Spika Tulia Ackson, ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye kipindi cha East Africa BreakFast cha East Africa Radio, wakati akijibu swali la juu ya kuonekana kuonesha nia ya kugombea Ubunge, kwenye jimbo la Mbeya Mjini.

"Mwenyezi Mungu akitupa Uhai 2020 nitagombea, ila nitagombea wapi? naomba watulie kwa sababu chama chetu kina utaratibu wake ila nashukuru ninavyoonekana nina uwezo wa kugombea maeneo mengi." amesema Tulia Ackson.

"Pale Mbeya Mjini kuna ofisi ya Tulia Trust, kwa hiyo wananchi wakisikia umefanya maeneo mengine, pale Mbeya maombi yanakuwa ni mengi, lakini kuhusu watu kufikiri mimi nataka Jimbo, siwezi kusema chochote." amesema Naibu Spika Tulia.

Naibu Spika Tulia Ackson ni miongoni mwa wadau wakubwa ambao wamejitokeza kuunga mkono, Kampeni ya Namthamini inayoendeshwa na East Africa Television na East Africa Radio, yenye lengo la kumsaidia binti aliyepo shuleni kupata taulo za kike, na tayari kwa miaka miatatu ya mwanzo imeshawafikia wanafunzi zaidi ya 5000.

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi