Jumapili , 27th Nov , 2016

Mgogoro unafukuta kuhusu matumizi ya tochi za kupimia mwendokasi wa madereva nchini Kenya, baada ya baadhi ya askari wa kikosi cha usalama barabarani nchini humo kudaiwa kutumia vipima mwendo hivyo kama mtego wa kuomba na kujipatia rushwa.

Wakizungumza kwa masikitiko makubwa, baadhi ya madereva wamesema tatizo limekuwa kubwa  baada ya kuanzishwa kwa faini za papo kwa papo mwezi mmoja uliopita na kwamba adhabu hizo hutozwa hata katika barabara ambazo hazina alama zinazoelekeza kiwango cha mwendokasi.

Baadhi ya barabara ambazo askari wa usalama barabarani hudaiwa kuchukua rushwa ni pamoja na ile ya Nairobi – Thika ambapo imedaiwa kuwa wanausalama hao hujificha porini wakirekodi mwendokasi wa magari na kisha kuwafuata madereva na kuomba rushwa.

 

________________
Kumpigia KURA msanii unayempenda kwenye #EATVAwards Bofya hapa https://www.eatv.tv/awards