Korosho
Hayo wameyabainisha katika mnada wa 8 kwa muungano wa wakulima kutoka wilaya tatu za Ruangwa, Nachingwea na Liwale (RUNALI) na kusema kwamba bei ya korosho mwaka huu imewatupa mkono hivyo wanahofia hata shughuli zao binafsi kukwama kwa kukosa fedha.
Nao viongozi katika Kijiji na Halmashauri hiyo, wamesema kwa hakika bei imeshuka lakini kwa mnada huo wa mwisho hali si mbaya sana, huku wanakijiji wakihusiwa kutumia fedha vizuri ili waepukane na balaa la njaa ambalo linahisiwa kuwepo hapo mwakani.