Baadhi ya mabasi ya abiria yanayofanya safari zake kati ya jiji la Dar es Salaam na mikoa ya kusini ya Lindi na Mtwara, yakiwa yamekwama eneo la Nyamwage mkoa wa Pwani kutokana na ubovu wa barabara.
Kaimu mkuu wa mkoa wa Lindi nchini Tanzania Agnes Hokororo ameisitisha kwa muda safari za Dar kwenda Lindi hadi Mtwara kufuatia kuharibika kwa barabara katika eneo la Marendego Pwani.