Beki za pembeni zaiumiza kichwa Yanga CAF
Yanga itakuwa dimbani Jumanne ijayo kuwavaa TP Mazembe katika mechi ya Kundi A ya Kombe la Shirikisho Afrika linaloandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika (Caf), hofu kubwa ya timu hiyo ni sehemu ya ulinzi wa pembeni beki ya kulia na beki ya kushoto.