Serikali kulifuta shirika la Ndege la Fast jet
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Anga nchini (TCAA) imesema Shirika la Ndege la fast jet kwa sasa halina hali nzuri na limepoteza sifa ya kuendelea na huduma hiyo, hivyo imetoa notisi ya siku 28 ya nia ya kulifuta kabisa shirika hilo.