Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais Samia aongoze hadi 2030 - Nape Nnauye

Saturday , 3rd Dec , 2022

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na mbunge wa Mtama Nape Nnauye amesema yeye ni miongoni mwa watu wanaopiga debe Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuchaguliwa katika uchaguzi wa 2025 hadi 2030 ili amalizie kazi ambayo ameianza

Nape ametoa kauli hiyo katika mjadala uliofanyika kwa njia ya mtandao (Zoom) ukiwakutanisha wadau mbalimbali kuhusu maendeleo ya mikoa ya kusini 

"Mimi ni katika wale wanaopiga debe wazi kabisa bila aibu, kwamba mama anastahili kuongezewa muda, akimaliza 2025 tumchague tena hadi 2030, tuna hakika akifika huko atakuwa ametufanyia kazi nzuri kwa mujibu wa katiba yetu atakuwa ndio wakati wa kupumzika" 

Aidha Nape amesema Rais Samia ameacha alama na amerudisha matumaini kwa watu waliokuwa wamepoteza matumaini 

"Rais Samia amerudisha matumaini mahali ambapo watu walianza kukata tamaa, amerudisha furaha mahali ambapo watu walianza kuvunjika moyo, amerudisha upendo mahali ambapo kulikuwa na chuki pengine, na ametuleta pamoja kama watanzania, jambo hili ni kubwa sana"

Kuhusu mikoa ya Lindi na Mtwara na maendeleo yake Nape amesema mikoa hiyo imeanza kupiga hatua kmaendeleo tofauti na watu wanavyoifikiria

"Mikoa ya Lindi na Mtwara ni mikoa ambayo kwa muda fulani hivi ilikuwa nyuma kimaendeleo na ni kwa sababu za kihistoria"

"Mimi jimbo langu la Mtama kwa miaka mitano tulikuwa tunapata fedha kidogo sana za ujenzi wa barabara, baada ya kuanzishwa kwa TARURA haikutengewa fedha ila Rais Samia alivyokuja akatenga fedha bungeni zikaja milioni 500 kwa majimbo yote"

Aidha mbunge wa Lindi Hamida Abdallah amesema serikali ya awamu ya sita imekuwa na kasi kubwa ya maendeleo ikiwemo upatikanaji wa maji safi na salama 

"Kwa kipindi hiki cha awamu ya sita tumeona kasi ya maendeleo inakuja kwa kasi kubwa sana, Lindi kulikuwa na changamoto kubwa sana ya upatikanaji wa maji safi na salama lakini serikali imeweka nguvu wametuoatia fedha zaidi ya bilioni 9" 

"Eneo ambalo limesahaulika ni Lindi mjini lakini ukiangalia namna ambavyo mji ulikuwa na sasa hivi ulivyo kumekuwa na mabadiliko makubwa, kumekuwa na barabara za lami, taa za barabarani na serikali imetuhakikishia fedha kwa ajili ya miradi ya kimkakati"

Kuhusu uwekezaji katika gesi Mkurugenzi Mkuu TPDC James Mataragio amesema ujio wa mradi wa LNG utaongeza pato la taifa na kukuza uchumi wa watanzania huku akiweka wazi kuwa tayari wananchi hususani mikoa ya kusini wameanza kuona matunda ya gesi 

"Mradi wa gesi wa LNG tunategemea utaleta mtaji wa kiasi cha dola za kimarekani bilioni 40, ni fedha nyingi sana na hivi karibuni mradi huu umekuwa namba moja kwa nchi hizi za kusini mwa Afrika" 

"Tayari nchi inafaidi uchumi wa gesi, mpaka leo tunapoongea asilimia 70 ya umeme wote unatumia gesi asilia, kwamba ule umeme unaozalishwa unatumia gesi asilia, ni kwamba tayari wananchi wa mikoa ya kusini wanafaidi matunda ya gesi" 

Mjadala huo pia umehudhuriwa na Mrajisi wa vyama vya ushirika na mtendaji Mkuu tume ya maendeleo ya ushirika Dkt Benson Ndiege na Mkurugenzi wa bodi ya Korosho Francis Alfred, 

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi