Dawa
NHIF imeeleza hayo kupitia taarifa yake kwa umma ambapo imeeleza kuwa hatua hiyo inaongeza wigo wa upatikanaji wa dawa kwa wanachama kwa kuzingatia miongozo ya tiba nchini.
Kutokana na maboresho hayo, Mfuko wa Taifa Bima ya Afya unawahakikishia wanachama wake kuwa huduma za matibabu zitaendelea kupatikana katika vituo vyote vilivyosajiliwa nchi nzima na endapo kutakuwa na changamoto za kiutekelezaji, mfuko umevishauri vituo vinavyotoa huduma viwasiliane na ofisi za mfuko huo kuepuka usumbufu usio wa lazima kwa wateja wao.