Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Matola aondoka Simba SC

Monday , 14th Nov , 2022

Uongozi wa Klabu ya Simba umethibitisha kuwa Kocha wao Msaidizi wa Simba, Seleman Matola ataondoka kwenye benchi la ufundi la timu hiyo kwa muda kwaajili ya kwenda kwenye kozi ya Ualimu ya leseni A ya CAF, itakayoanza Novemba 21 mwaka huu.

Taarifa hiyo imethibitishwa na Meneja wa Mawasiliano Simba SC, Ahmedy Ally ambaye amesema, wanafurahi kwa hatua hiyo kwani Matola akiimaliza kozi hiyo basi atakuwa atapanda daraja na kuruhusiwa kuwa Kocha Mkuu katika vilabu vya Ligi kuu.

''Ni kweli tumepokea maombi kutoka kwake na hii ni fursa kwake kwenda kujiongeza katika idara ya elimu , sisi Simba tunamtakia kila la kheri'' amesema Ahmedy Ally.

Mabosi wa Simba watalazimika sasa kuboresha benchi la ufundi kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma kocha huyo alipokwenda kusoma timu ikiwa chini ya Didier Gomes ambapo alitafutiwa msaidizi wake Thierry Hitimana na baadaye Matola aliungana nao alipomaliza masomo yake.

Simba inatarajiwa kushuka dimbani Jumatano ya Novemba 16 mwaka huu kucheza mchezo wa Ligi Kuu NBC Tanzania dhidi ya Namungo katika uwanjna wa Benjamin Mkapa majira ya saa moja usiku .
 

HABARI ZAIDI

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini