Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Parimatch yaidhamini Mbeya City kwa msimu 2022/23

Tuesday , 9th Aug , 2022

Kampuni ya michezo ya kubashiri mtandaoni ya Parimatch imetangaza kuingia makubaliano ya kuidhamini klabu ya Mbeya City kwa msimu wa 2022/23.

Makabidhiano ya jezi kama ishara ya udhamini wa kampuni ya Parimatch katika klabu ya Mbeya City

Hatua hiyo ni muendelezo wa udhamini wao kwa klabu hiyo kama ilivyofanya kwa msimu 2021/22, ambapo Afisa Habari wa kampuni hiyo Ismael Mohamed amesema wamefikia hatua hiyo kutokana na ukubwa wa Mbeya City na idadi ya mashabiki walionao.

"Mbeya City ni moja ya klabu kubwa kwa hapa Tanzania hususani ukiangalia idadi ya mashabiki na ushawishi katika soka na hiyo ndio sababu tosha ya sisi kurejea tena kufanya udhamini na Mbeya City kwa msimu huu mpya, kama mtakumbuka vizuri msimu wa 2020/2021 tulikuwa wadhamini wakuu kwa mara ya kwanza", amesema Ismail.

"Sisi kama Parimatch Moja ya jukumu letu kubwa ni kuhakikisha michezo inakua kuanzia ngazi ya chini hadi ngazi ya kimataifa. Lakini pia tunaendelea na michakato mablimbali ya kuunga mkono vilabu vingine kutoka ligi kuu,  ligi daraja la kwanza na hata Vilabu Chipukizi . Ikiwa ni kuunga mkono juhudi za TFF na bodi ya ligi kuhakikisha ligi za Tanzania zinakuwa na tunaenda Kimataifa", ameongeza.

Pamoja na kutoa pesa taslimu kwa timu hiyo, pia Parimatch pia itatoa vifaa kwa klabu pamoja na ukarabati mdogo wa uwanja wa Sokoine hasa katika eneo la kukaa la benchi la ufundi  kwa awamu.

Kwa upande wa Mtendaji Mkuu wa Mbeya City Emmanuel Kimbe amewashukuru kampuni ya Parimatch Tanzania kwa kusaini tena mkataba na timu hiyo huku kwa niaba ya klabu ya Mbeya City akiwaahidi klabu hiyo watatekeleza matakwa yote ya kimkataba yaliyopo kwenye mkataba huo.

Parimatch ni kampuni inayoendesha shughuli za michezo ya kubashiri mtandaoni ikiwa imesajiliwa na bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania kwa takriban miaka 5 sasa. Kimataifa ipo zaidi ya nchi 15 ikiwa na wateja zaidi ya milioni moja duniani kote.

 

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi