Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ten Hag amtaka Ronaldo kujiimarisha kwanza

Thursday , 4th Aug , 2022

Kocha wa Manchester United Erik Ten Hag amesema Cristiano Ronaldo anaweza kufaa katika aina yake ya uchezaji lakini atahitaji kujiimarisha kwanza kabla ya kupata nafasi ya kuthibitisha kuwa anastahili nafasi katika kikosi cha kwanza.

Kocha Erik Ten Hag akimwelekeza jambo Ronaldo katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Rayo Vallecano jumapili iliyopita.

Ronaldo hakuwepo katika kikosi cha United kwenye ziara ya maandalizi ya msimu mpya nchini Thailand na Australia, na pia alikosekana katika mchezo wa kirafiki waliofungwa goli 1 kwa 0 dhidi ya Atletico Madrid, lakini alicheza dakika 45 za kipindi cha kwanza katika mchezo dhidi ya Rayo Vallecano uliomalizika kwa sare ya goli 1 kwa 1 katika dimba la Old Trafford Jumapili iliyopita.

Ten Hag aliongeza kusema mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno anaweza kufaa katika mfumo wake wa jinsi anavyotaka United icheze ila kwanza inabidi ajiimarishe kimwili na aonyeshe kwamba anaweza kutimiza majukumu ipasavyo.

Mustakabali wa Ronaldo ndani ya United umekuwa wa hali ya sintofahamu baada ya vyombo vya habari vya Uingereza kuripoti kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 aliomba kuondoka klabuni hapo ili acheze ligi ya mabingwa barani Ulaya.

United ambayo itacheza ligi ya Europa msimu huu, wataanza kinyang’anyiro cha ligi kuu ya Uingereza siku ya Jumapili dhidi ya Brighton & Hove Albion.

HABARI ZAIDI

Bw. Nazar Nicholas (katikati) akikabiziwa tuzo ya WSIS 2024

Tanzania yashinda Tuzo WSIS 2024, nchini Uswisi

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton