Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanahabari watakiwa kupata elimu ya ukatili

Tuesday , 17th May , 2022

Katibu Mkuu wa Katiba na Sheria, Bi. Mary Makondo amewataka wahariri  na waandishi wa habari kupata mafunzo maalumu kuhusu kuripoti taarifa zinazohusiana na vitendo vya ukatili wa kijinsia katika jamii zetu.

Amesema hayo wakati wa  ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili ya namna ya utoaji taarifa za ukatili wa kijinsia kwa Wahariri na Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini , mafunzo yaliyofanyika jijini Arusha.

Bi. Makondo amesema lengo la mafunzo hayo ni kujengeana uwezo, kujifunza, kubadilishana uzoefu, mbinu na kujadiliana kuhusu nafasi ya Waandishi wa Habari na Wahariri katika kutokomeza ukatili wa kijinsia katika jamii zetu.

Bi. Makondo amesema kumekuwa na ongezeko la matukio ya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia na uhalifu kama vile, ubakaji, ndoa za utotoni, ukeketaji, ukatili wa majumbani, wajane kupokwa mali za wenza wao na mauaji. 

"Katika kukabiliana na ukatili wa kijinsia, Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wadau wake katika mapambano hayo. Miongoni mwa hatua hizo ni pamoja na kuimarisha mifumo ya kisheria na utoaji haki, huduma za afya, elimu, kuanzisha vituo vya huduma kwa manusura wa ukatili na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola, ikiwemo mahakamani wote wanaotuhumiwa na makosa ya ukatili. " amesema Bi. Makondo. 

Aidha, Serikali imewezesha kutungwa kwa sheria ya Msaada wa kisheria kwa lengo la kumeimarisha upatikanaji haki kwa watu wasio na uwezo wa kumudu gharama za mawakili. Kwa sasa Wananchi wana uwezo wa kutafuta na kupata afua za kisheria kwa kutumia njia mbadala za utatuzi wa migogoro nje ya Mahakama. Haya yote ni juhudi za Serikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria na kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Wahariri na Waandishi wa habari.

Bi. Makondo ametoa rai kwa Wanahabari kuzingatia maadili ya uandishi na kulinda waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia wakati wa utoaji taarifa ili kuepuka athari zaidi kwa wahanga wa matukio haya.

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi