Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TAKUKURU yaokoa mamilioni ya NHIF

Wednesday , 3rd Feb , 2021

TAKUKURU mkoa wa Kagera imekabidhi zaidi ya shilingi milioni 10.3 kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), zilizolipwa kwa udanganyifu kwenye maduka mawili ya dawa za binadamu ambayo ni MK Pharmacy na EJU Pharmacy, baada ya kuwasilisha nyaraka za madeni wakidai kutoa huduma kwa wagonjwa.

Fedha zilizokabidhiwa na TAKUKURU kwa Mkuu wa mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali Marco Gaguti.

Akikabidhi fedha hizo mbele ya mkuu wa mkoa wa Kagera, mkuu wa TAKUKURU wa mkoa huo John Joseph, amesema kuwa fedha zilizokabidhiwa ni sehemu ya shilingi milioni 304, ambazo taasisi hiyo imeziokoa kama madeni hewa, kutokana na nyaraka zilizotumika kubainika kuwa zimeghushiwa.

Joseph amesema kuwa ufuatiliaji umebaini kuwa madai hayo yalikuwa ni ya uongo, kwa kuwa fomu za NHIF zilizowasilishwa ziliandikwa na mtu aliyeitwa Dk. Frida Samwel, ambaye sio daktari na wala hakuwahi kuajiriwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa na hatambuliki.

Akizungumzia tukio hilo mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti, amesema kuwa serikali haitavumilia vitendo vyovyote vya ubadhirifu, na kwamba uchunguzi dhidi ya tukio hilo unaendelea na watakaobainika watachukuliwa hatua za kisheria.

 

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu