Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TAKUKURU yaokoa mamilioni ya NHIF

Wednesday , 3rd Feb , 2021

TAKUKURU mkoa wa Kagera imekabidhi zaidi ya shilingi milioni 10.3 kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), zilizolipwa kwa udanganyifu kwenye maduka mawili ya dawa za binadamu ambayo ni MK Pharmacy na EJU Pharmacy, baada ya kuwasilisha nyaraka za madeni wakidai kutoa huduma kwa wagonjwa.

Fedha zilizokabidhiwa na TAKUKURU kwa Mkuu wa mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali Marco Gaguti.

Akikabidhi fedha hizo mbele ya mkuu wa mkoa wa Kagera, mkuu wa TAKUKURU wa mkoa huo John Joseph, amesema kuwa fedha zilizokabidhiwa ni sehemu ya shilingi milioni 304, ambazo taasisi hiyo imeziokoa kama madeni hewa, kutokana na nyaraka zilizotumika kubainika kuwa zimeghushiwa.

Joseph amesema kuwa ufuatiliaji umebaini kuwa madai hayo yalikuwa ni ya uongo, kwa kuwa fomu za NHIF zilizowasilishwa ziliandikwa na mtu aliyeitwa Dk. Frida Samwel, ambaye sio daktari na wala hakuwahi kuajiriwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa na hatambuliki.

Akizungumzia tukio hilo mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti, amesema kuwa serikali haitavumilia vitendo vyovyote vya ubadhirifu, na kwamba uchunguzi dhidi ya tukio hilo unaendelea na watakaobainika watachukuliwa hatua za kisheria.

 

HABARI ZAIDI

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro