Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ijue sababu ya akili za watu kuota vitambi

Monday , 4th Jan , 2021

Mhamasishaji Paul Mashauri, amesema kuwa akili za watu wengi kwa sasa zimeota vitambi kwa sababu wanaruhusu milango yao ya fahamu ipitishe kila kitu wanachokisikia, hali inayopelekea ubongo wao kuwa na uchafu mwingi.

Paul Mashauri, Mhamasishaji

Kauli hiyo ameitoa hii leo Januari 4, 2021, wakati akizungumza kwenye kipindi cha SupaBreakfast cha East Africa Radio, na kueleza kuwa kila mtu mwenye akili anatakiwa kuweka malengo na si kukaririshwa kuwa mtu hawezi kusimama bila mtu mwingine.

"Watu wengi wana vitambi kwenye akili zao kwa sababu wanaruhusu milango yao ya fahamu kuingiza kila kitu kwenye ubongo wao, matokeo yake wana uchafu mwingi kwenye ubongo, ndiyo maana unakuta watu wanawaza tu ngono na vitu negative kwa sababu ndivyo walivyoviingiza", amesema Mashauri.

Aidha Mashauri ameongeza kuwa, "Hakuna mtu 'single', wewe una mwili, una nafsi na roho na nafsi yako ina vitu vitatu, ina utashi, ina hisia na ina fikra, kwahiyo tayari wewe ni jeshi la mtu mmoja na ndani ya nafsi yako unaweza kuwasiliana na hivyo vitatu na mkakubaliana".

"Shida ni kwamba watu wengi wameaminishwa kwamba wanahitaji watu wengine ili waweze kutoka lakini si kweli unaanza na wewe, unapokuwa unajua unaelekea wapi tutaweza kukutofautisha wewe na wanyama na mimea ukiweka malengo sababu wewe una utambuzi na ufahamu", amesisitiza.

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu