Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Siwezi kumlazimisha Sugu anikabidhi ofisi"- Tulia

Monday , 23rd Nov , 2020

Mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini, Dk. Tulia Ackson, ameanza utaratibu wa kusikiliza kero za wananchi, ambapo kila Alhamisi atakuwa anasikiliza kero mbalimbali katika ofisi yake iliyoko kwa mkuu wa wilaya ya Mbeya na kila Jumamosi atakuwa kwenye ofisi zake zilizopo Uyole.

Kushoto ni mbunge wa Mbeya Mjini kupitia CCM, Dkt. Tulia Ackson, na kulia ni mbunge mstaafu wa jimbo hilo kupitia CHADEMA, Joseph Mbilinyi (Sugu).

Dkt. Tulia ameitoa hii leo Novemba 23, 2020, wakati akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake, na kusema kuwa hiyo ni moja ya ahadi yake aliyoitoa wakati wa kampeni kwamba atahakikisha anatenga muda wa kukutana mwananchi mmoja mmoja ili asikilize kero zake.

"Nimeanza utaratibu wa kusikiliza kero za wananchi wangu kila mwenye shida yeyote afike kwa kulingana na siku nilizozianisha," amesema Dkt. Tulia.

Akizungumzia suala la kukabidhiwa ofisi na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia CHADEMA, Joseph Mbilinyi, maarufu kama Sugu, Dk. Tulia, amesema kuwa hakuna chochote kilichofanyika kati yake na mtangulizi wake huyo aliyekuwa anatumia Ofisi za Ardhi.

"Hadi sasa hakuna makabidhiano na mbunge mstaafu, Joseph Mbilinyi, siwezi kumlazimisha, mimi nimejiandaa kikamilifu kuwatumikia wananchi siwezi kusubiri kwa sababu naona hajihusishi na chochote na ni mlolongo mrefu, ndiyo maana hata ofisi natumia nyingine", ameongeza Dkt.Tulia.

HABARI ZAIDI

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini