Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Baraka Sadick ataja sababu ya ubora wake

Saturday , 25th Aug , 2018

Licha ya kimo cha nyota wa timu ya Kikapu ya Mchenga Bball Stars Baraka Sadick kuwa kifupi, lakini kiwango chake kimekuwa tishio kwenye michuano ya Sprite Bball Kings  hasa kwenye game mbili za fainali ambazo ameongoza kwa pointi.

Mchezaji Baraka Sadick akikimbia na mpira kwenye game 1.

Akiongea kwenye 'FNL' ya East Africa Television Ijumaa usiku Agosti 24, Baraka amesema kujituma, kufanya mazoezi zaidi hususani ya 'kushoot' ndio kitu kimemfanya awe bora akichangiwa na maandalizi mazuri ya timu yake.

''Kwanza ili ufanye vizuri kwenye Kikapu mazoezi ni lazima, kwasababu unaweza ukawa mrefu lakini mzembe, hivyo unatakiwa kujijenga katika misingi ya Kikapu na hiyo ndio siri ya kuwa bora ukiacha maandalizi ya timu kiujumla ambayo nayo yanamchango mkubwa'', amesema Baraka.

Kwa upande wake nyota wa Flying Dribblers Baraka Mopele ambaye yeye na timu yake wapo nyuma kwa game mbili za mwanzo kwenye 'best of five' amesema watajitahidi kutumia nafasi kwenye game 3 ambayo inapigwa leo kwenye uwanja wa taifa wa ndani kuanzia saa 10:00 jioni.

Mchezaji Baraka Mopele wa Flying Dribblers akiifungia timu yake.

Baraka ameeleza tatizo kubwa ambalo wamekuwa wakifanya ni kutotumia vizuri nafasi wanazotengeneza na tayari wamesharudi chini na kulifanyia mazoezi eneo la 'kushoot' ili waweze kupata pointi nyingi kwenye game 3 na hatimaye kushinda game hiyo na game 4 ili wacheze game 5.

Mpaka sasa Baraka Sadick wa Mchenga amefunga pointi 174 huku Baraka Mopele wa Flying Dribblers akiwa amefunga pointi 134. Endapo Mchenga leo watashinda watajitwalia milioni 10 na kombe na kuwaacha Flying Dribblers wakijikusanyia milioni 3 na 'MVP' ataweka mfukoni kiasi cha shilingi milioni 2.
 

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi