Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simu ya Nondo ilikuwa ikitumika alipotekwa

Friday , 18th May , 2018

Shahidi katika kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi nchini, Abdul Nondo, amesema kuwa simu ya mtuhumiwa ilikuwa inatumika kipindi alichokuwa anadai kwamba ametekwa.

Shahidi huyo ambaye amejulikana kwa jina la Abdul Kareem anayehusika katika kitengo cha makosa ya mtandao amesema kuwa simu ya Nondo ilikuwa ikitumika katika kipindi ambacho Mtuhumiwa alikuwa akidai ametekwa ingawa ameshindwa kuelezea ilikuwa ikitumika na nani kwa madai kuwa hana uwezo huo.

Akizungumza na www.eatv.tv Wakili wa Abdul Nondo, B. Jebra Kambole amesema kwamba mbali na Shahidi Abdul Kareem, Koplo John ambaye ni mpelelezi katika kesi hiyo ametoa ushahidi wake ambao ni maelezo ya Nondo aliyoyatoa katika kituo cha polisi Iringa.

Wakili Kambole amesema kwamba licha ya serikali kuwa na mashahidi watano katika kesi hiyo, Juni 12-13 inategemea kuwepo na mashahidi wengine ambao bado hawajajulikana watakuwa wangapi.

Hakimu katika kesi hiyo John Mpitanjia ameahirisha kesi hiyo mpaka Juni 12 ambapo Mtuhumiwa Abdul Nondo ataendelea kuwa nje kwa dhamana.

Nondo anatuhumiwa kwa makosa mawili Kosa la kwanza ni kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni Machi 7, 2018 akiwa Ubungo na kusambaza kwa kutumia mtandao wa WhatsApp kuwa yupo hatarini, kosa la pili ni kutoa taarifa za uongo akiwa mjini Mafinga kwa askari Polisi wa kituo cha Mafinga Wilayani Mufindi.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton