Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ratiba kuagwa wanafunzi wa UDSM kesho

Wednesday , 13th Jun , 2018

Uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM), imetoa taarifa ya kukatisha ratiba ya masomo kwa muda wa masaa matatu kesho Juni 14, 2018 ili kutenga muda wa kuaga miili ya waliokuwa wanafunzi na watumishi wa chuo hicho.

Taarifa hiyo imetolewa leo Juni 13, 2018 na Ofisi ya Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma Profesa Bonaventure Rutinwa na kuongeza kuwa masomo yatasitishwa kuanzia Saa 4:00 asubuhi mpaka 7:00 Mchana.

Taratibu za kuaga miili ya marehemu zitafanyika katika ukumbi wa Nkrumah uliopo chuoni hapo siku ya kesho Juni 14, 2018 kuanzia Saa 4:00 Asubuhi.

Katika ratiba ya kutoa heshima za mwisho kwa marehemu hao inaonesha, waombolezaji wataanza kuingia katika ukumbi wa Nkrumah kuanzia saa 3:00 asubuhi, na ikifika 3:45 miili ya marehemu hao itaingia ukumbini, ambapo shughuli ya kuaga itaanza rasmi saa 5:40 asubuhi mpaka 6:50 Mchana.

Juni 11, 2018 katika eneo la Riverside-Ubungo wanafunzi wawili na watumishi wawili wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM), walifariki Dunia baada ya gari la wagonjwa walilokuwa wamepanda kugoganga na lori la mizigo walipokuwa wanaenda katika Hospitali ya Chuo hicho kwa matibabu.

Waliofariki kutokana na ajali hiyo ni wanafunzi Erasto Sango Steven na Mary Godian Soko na watumishi wawili James Rutayuge ambaye alikuwa ni dereva pamoja na muuguzi msaidizi daraja la pili Jonathan Lung’ando.

 

 

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi