Hakimu mfawidhi wa Mahakama hiyo James Karayemaha amesema anahitaji majibu hayo mnamo Marchi 5 mwaka 2018 siku ambayo mtuhumiwa huyo atafikishwa Mahakamani ikiwa ni baada ya agizo la mtuhumiwa huyo kupimwa akili kutotekelezwa hapo awali.
Nabii Tito Machibya alifikishwa Mahakamani hapo akituhumiwa kufanya uchochezi wa kidini kupitia mafundisho anayo yatoa na amekuwa akiieleza Mahakama kuwa amekuwa akifanya hivyo kwa sababu ana matatizo ya akili na kutoa vithibitisho toka hospitali ya Taifa Muhimbili.