Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Magufuli ameweza kuitikisa Afrika- Polepole

Sunday , 24th Sep , 2017

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amefunguka kwa kumsifia Rais John Magufuli kwamba ni mwanaume pekee aliyeweza kuifanya Afrika nzima ikazizima kwa kuweza kupinga vitendo vya unyonyaji kwa taifa la Tanzania.

Polepole ameeleza hayo kupitia ukurasa wake maalumu wa facebook mchana wa leo huku akinukuu baadhi maneno aliyowahi kuyatoa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ambayo yalikuwa wazi kabisa yakiongelea namna ya kujikomboa ili bara la Afrika kiujumla liweze kufikia uhuru wake wa kiuchumi.

"Leo Afrika nzima inazizima kwamba yuko mwanaume ambaye ameweza kusema imetosha 'enough is enough' siyo haki na ni unyonyaji kuchukua madini yetu katika namna ambayo haki yetu inapokwa. Ndugu Magufuli ana amini sana katika sekta binafsi na hasa katika ujenzi wa uchumi wa viwanda sambamba na sekta ya umma. Lakini ana amini zaidi katika sekta binafsi inayojiendesha kwa kanuni za maadili ikiwemo kulipa kodi. Anaamini katika uwekezaji kutoka nje, lakini unaotambua kwamba sisi ni taifa huru na tunayo haki ya kunufaika kutokana na utajiri wa rasilimali zetu", ameandika Polepole.

Aidha, Polepole amesema CCM imemleta Rais Magufuli katika wakati muafaka ambapo nchi ilikuwa inaelekea pabaya.

"Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemleta ndugu Magufuli wakati muafaka wakati tunamuhitaji zaidi mtu kama yeye. Ukisoma maelezo na nukuu za Mwalimu Nyerere katika maelezo yangu ya awali juu ya maono ya Mwalimu Nyerere utaungana nami kusema ile aina ya uongozi mpya katika bara la Afrika, Tanzania tumekuwa kinara wa kwanza na wengine watafuata ili bara la Afrika lirejeshe heshima yake ya uhalisia na asili", amesisitiza Polepole.

Kwa upande mwingine, Polepole amesema ipo siku ataeleza ni kwanini Rais Magufuli amekuwa zawadi katika taifa la Tanzania kwenye kipindi hiki.

 

 

HABARI ZAIDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa January Makamba

Ziara ya Rais Samia Korea kuanza rasmi Mei 31 2024

Bw. Nazar Nicholas (katikati) akikabiziwa tuzo ya WSIS 2024

Tanzania yashinda Tuzo WSIS 2024, nchini Uswisi

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20