Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Gambo kutoa ushahidi kesi ya Lema na mkewe

Wednesday , 18th Jan , 2017

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo pamoja na mashahidi wenzake wanne wanatarajia kutoa ushahidi katika kesi inayomkabili Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema pamoja na na Mkewe Neema Lema, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, Februari 3, 2017

Godbless Lema (Kushoto) na Mkewe Neema

Kwa mujibu wa Wakili wa Serikali Alice Mtenga amesema licha ya Gambo pamoja na wenzake wanne kutoa ushahidi wao Februari 3 mwaka huu, pia mashahidi hao watakuwa na vielelezo vitatu vitakavyotolewa mahakamani hapo.

Mtenga amesema hayo mbele ya Hakimu, Nestory Barro wakati akiwasomea maelezo ya awali washtakiwa hao ambao ni mume na mke.

Amesema mashahidi watano watatoa ushahidi wao ambao ni Mkuu wa Mkoa Arusha Mrisho Gambo , Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Arusha(RCO) ,George Katabazi, (ASP) Damasi Massawe, mhusika kutoka kampuni ya simu ya Vodacom pamoja na mtaalam wa picha.

Pia amevitaja vielelezo watakavyovitoa katika kesi hiyo kuwa ni nakala ya taarifa za mawasiliano ya simu kutoka kampuni ya Vodacom, Simu ya mshitakiwa ambaye ni ya mke wa Lema ,Neema Lema pamoja na taarifa ya uchunguzi kutoka kitengo kinachoshughulikia masuala ya kiuchunguzi (Forensic Bureau).

Mrisho Gambo Mkuu wa Mkoa wa Arusha

Baada ya kuwasomea maelezo hayo ya awali, washtakiwa hao kwa pamoja walikiri kuwa ni wakazi wa Arusha na Lema ni Mbunge wa Arusha Mjini ila walikataa kusambaza ujumbe huo wa kumtukana Gambo wala tarehe ya kukamatwa kwao.

Naye Hakimu Barro ameahirisha kesi hiyo hadi Februari 3 mwaka huu, ambapo Gambo atafika mahakamani hapo kutoa ushahidi wake ili kuithbitishia mahakama jinsi aliyojisikia vibaya, baada ya kutukanwa na Lema pamoja na Mke wake Neema.

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi