Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Dkt. Mengi kuja na kiwanda cha magari

Tuesday , 20th Nov , 2018

Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dk. Reginald Mengi leo ametia saini mkataba wa makubaliano baina ya IPP Automobile Ltd na kampuni ya Youngsan Glonet Corporation ya Korea Kusini kwa ajili ya uanzishaji wa kiwanda cha kuunganisha magari nchini kitakachoanza kazi mwakani.

Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dkt. Reginald Mengi.

Dk. Mengi amesema kuwa uwekezaji huo utagharimu dola za Mareklani milioni 10 sawa na shilingi bilioni 22 za Tanzania na kusema kuwa katika kipindi cha mwezi Oktoba mwakani gari la kwanza litatolewa katika kiwanda hicho cha IPP Automobile kitakachojengwa eneo la Kurasini Jijini Dar es Salaam.

"Kiwanda cha IPP Automobile Limited kwa kushirikiana na kampuni ya Youngsan Glonet Corporation (KOTA) kinatarajia kuunda magari aina ya Kia, Hyundai na Daewoo, ambapo kati ya September na October mwaka 2019 Tanzania itaanza kutumia gari la kwanza", amesema Dkt. Mengi.

Shughuli ya utiaji saini makubaliano hayo imefanyika Ofisi za Makao Makuu ya IPP Dar es Salaam ambapo, Dk. Mengi amesema kuwa kiwanda hicho kinatarajiwa kuzalisha magari 1,000 ya aina tatu na kutoa ajira rasmi kwa watu 500 na zisizo rasmi zaidi ya 1000.

Kwa upande wake balozi wa Korea nchini Tanzania Song Geum Young amesema kuanzishwa kwa kiwanda hicho ni katika utekelezaji wa sera ya Tanzania ya Viwanda na kuongeza kuwa kitasaidia kuongeza ajira pamoja na mapato kwa nchi.

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu