LHRC yalikosoa bunge la Tanzania kukosa sifa

Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania linaloelekea kumaliza muda wake limetajwa kugubikwa na kasoro nyingi zilizopelekea wananchi kukosa Imani na Bunge hilo na hivyo kupoteza sifa ya kuwa chombo cha uwakilishi wa wananchi.

Akizungumza na East Africa Radio mwanasheria Hamisi Mkindi kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kitengo cha ufuatiliaji Bunge na chaguzi mbalimbali, amezitaja kasoro hizo kuwa ni pamoja na lugha chafu za matusi zilizopelekea Bunge kupoteza heshima yake mbele ya jamii

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS