Rais Samia aandika Historia Angola
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, ameendelea kung’ara katika jukwaa la kimataifa kwa kuanza ziara ya kihistoria ya siku tatu nchini Angola, kuanzia Aprili 7 hadi Aprili 9, kwa mwaliko rasmi wa Rais wa Angola, Mhe. João Lourenço.