Jambo Squad kuibuka na Digidigi
Kundi la muziki la Jambo Squad maarufu kama Mamong'oo wamesema baada ya kukaa kimya kutokana na matatizo binafsi na masuala ya uchaguzi wamejipanga kurudi kwa kishindo mwaka huu na wapo mbioni kuachia video ya ngoma yao walioipa jina la Digidigi.
