Serikali yasisitiza kufuta tozo 5 kwenye korosho
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema uamuzi wa Serikali kufuta tozo tano kati ya tisa alizokuwa anakatwa mkulima wa zao la korosho uko pale pale na unatarajiwa kuanza kutumika katika msimu mwaka huu hivyo ameitaka Bodi ya Korosho kusimamia uamuzi huo.

