Madiwani wamtupia lawama Mkurugenzi Mvomero
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro Florent Kyombo, ametuhumiwa na baraza la madiwani kuwa anatumia vibaya madaraka yake kutokana na kufanya ubadhirifu wa fedha za halmashauri hiyo kiasi cha shilingi milioni 120.

