"Tumshukuru Mungu kuzaliwa Tanzania" - Jerry Muro
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro ametaka watanzania kuthamini uwepo wa rasilimali za Wanyamapori pamoja na uoto wa asili katika maeneo ya hifadhi za taifa, kwa kujenga utamaduni wa kutembelea maeneo hayo ili kujifunza umuhimu na nafasi ya uhifadhi katika mchango wa pato la Taifa.