CCM yapiga marufuku matarumbeta
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole, amesema kuwa wagombea wa nafasi mbalimbali katika uchaguzi ujao, hawapaswi kutumia matarumbeta wakati wanaenda kuchukua fomu za ugombea, badala yake waende kimya kimya na matarumbeta yatapigwa mara baada ya chama kumteua mgombea.