Ahukumiwa miaka 3 kwa kutoa hongo ya laki 1
Mahakama ya Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza, imemhukumu kifungo cha miaka mitatu au kulipa faini ya Shilingi laki nane raia mmoja wa China, anayekabiliwa na shtaka la kutoa rushwa kiasi cha shilingi laki moja ili arejeshewe mashine yake ya kuchezeshea mchezo wa bahati nasibu.

