RPC azungumzia mauaji ya M/Kiti wa BAWACHA
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Gilles Muroto, amesema kuwa tayari jeshi hilo limemkamata mtuhumiwa wa mauaji ya Mwenyekiti wa BAWACHA Kata ya Palanga Asia Said, aliyeuawa baada ya kuchomwa mshale usiku wa kuamkia leo wakati akiandaa chakula cha jioni yeye na mume wake.

